

Unique Fashion tupo barabara ya NairobiTriple Complex, Moshi.8 Desemba 2011
K.K.K.T DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI KONGAMANO KUU LA VIJANA KIBAHA FILBERT LIKIPAMBWA NA WAIMBAJI WA NYIIMBO ZA INJILI GLORIOUS CELEBRATION.
Kongamano hili limeandaliwa na vijana Kibaha katika shule ya sekondari ya Filbert. Kongamano hili limebeba ujumbe kutoka Daniel 5-14 unaosema, "Nimesikia Habari Zako Kwamba Roho wa Mungu Iko Ndani Yako, na Kwamba Nuru na ufahamu wa Akili Bora Zimeonekana Kwako"
Kutoka kushoto nimchungaji Anthon, Chase Msinga, Mwenyekiti wa Vijana Oscar Mnyirenda
Katibu wa Vijana, Amoni akiwakaribisha Glorious Celebration stejini kwaajili ya uimbaji.
Glorious Celebration wakilitawala jukwaa siku ya kwa kuita uwepo wa Mungu kwa njia ya uimbaji.
Meneja wa masoko wa Glorious Celebration, (aliyevalia penzi) akiwa na mpigaji gitaa wa Glorious, Imma Base wakisubilia chakula cha mchana.
Dada Nice akimwimbia Mungu siku ya Vijana Kibaha. Wengine kuanzia kulia ni Davina, Mercy, Chaka, Lisper na Mercy.
Wapigaji vyombo wakihusika katika kumtumikia Mungu
David akifanya kazi ya Bwana na kutoa mchango wake wa uimbaji kwa hisia kali
Kutoka kulia ni OG na Ima Base
Kiongozi wa kikundi cha Glorious Celebration akiimba siku ya Vijana Kibaha
Vijana wa Kibaha wakimtukuza Mungu
Baadhi ya Vijana waliohudhuria katika kongamano la Vijana Kibaha katika shule ya sekondari Filbert Bayi
Vijana wa KKKT wakiwasikiliza waimbaji wa nyimbo za injili GC
Hii ilikuwa ni siku furaha na shangwe kwa vijana wa Kibaha.
Baadhi ya waimbaji wa kikundi cha Glorious Celebration wakipata chakula cha mchana baada ya uimbaji
Baadhi ya uimbaji wa Glorious Celebration wakiwa katika kipindi cha michezo baada ya kutoka katika huduma ya uimbaji katika kongamano la Vijana Kibaha
USHUHUDA WA MCHUNGAJI HARISON MMANYI KABLA NA BAADA YA WOKOVU
Mchungaji Harison Mmanyi, akiwaombea watu waliokoka katika kongamano la vijana Kibaha
Mchungaji, Harison Mmanyi atoa ushuhuda wake kuhusu maisha yake kabla na baada ya wokovu.
Kabla ya wokovu alikuwa ni mlevi na alijulikana sana katika mabaa mengi hapa jijini Dar es Salaam.
Mungu alizungumza naye na baadae aliamua kuokoka. Akiwa katika wokovu Mchungaji huyu alikuwa ni Meneja wa Kampuni ya Konyagi nchini Tanzania, na baadae akaendelea na wokovu akiwa bado ni meneja wa kampuni hiyo.
Baada ya kuokoka aliomba Mungu amuondoe katika kampuni hiyo, lakini haikuwezekana kutokana ujumbe aliopata kwa Mungu kwamba hataondoka mpaka lengo lake MUNGU litimie. Lengo a Mungu lilikuwa kumtumia akiwa katika kampuni hiyo kuwaokoa wengine. Baadae Mungu akamtoa katika kampuni hiyo.
Maisha yaakanza kuwa magumu akiwa katika huduma, akamua kujihusisha na biashara ya kuku na hakufanikiwa Mchungaji huyo akieleza kwa uchungu mkubwa kutokana na kufilisika kwake ambapo ilifika hatua ya kumtegemea mke wake kwa kila kitu.
Mungu akaanza kufungua milango kutoka na uvumilivu wake katika kutumikia Mungu. Fedha na mali zikaanza kuja kwa wingi, na mpaka sasa amebarikiwa na anasomesha watoto wake ma watoto wa watoto wa ndugu zake..
Akielezea kusudu la Mungu kuhusiana na kufilisika kwake, anasema Mungu alipenda apoteze mali zake zote alizochuma akiwa katika kampuni ya konyagi, ili kumuonyesha kuwa Mungu anaweza kumtoa mtu kuanzia chini kabisa na kumuinua juu.
Posted by Rulea Sanga
MWISHO
----------------------------------------------------------------------------------
MWISHO






